MAGUFULI AWAPA SAVU SIMBA NA YANGA

MAGUFULI AWAPA SAVU SIMBA NA YANGA



Mgombea urais kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk John Magufuli, amewaahidi wanamichezo kuwa, endapo atapata nafasi ya kuwa rais, atahakikisha anaweka mikakati ya kuzisaidia timu za hapa nchini zikiwemo Yanga, Simba na Taifa Stars kuhakikisha zinakuwa mabingwa wa Afrika. Magufuli alisema hayo juzi Jumatano alipokuwa kwenye mkutano wa kampeni za kuomba kura za urais zilizofanyika katika Uwanja wa Kawawa uliopo Kigoma Ujiji.