ALICHOKISEMA LOWASSA KUHUSU MABOMU

ALICHOKISEMA LOWASSA KUHUSU MABOMU








Mgombea urais kwa tiketi ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) anayeungwa mkono pia na Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa), Edward Lowassa, ameelezea kusikitishwa na hatua ya polisi jijini Tanga kuwapiga mabomu wananchi waliokuwa wakirejea makwao kutoka katika mkutano wake wa kampeni juzi.



ALICHOKISEMA HIKI HAPA

“Niliporejea hotelini baada ya mkutano jana (juzi), nilipata taarifa kwamba polisi waliwapiga mabomu wafuasi wa Ukawa, nasikitika sana kwa kitendo kile, kwa sababu tulikubaliana polisi wasipige watu mabomu,” alisema akiwataka washirikiane na polisi kufanya kazi pamoja.
Aliyasema hayo alipokuwa akizungumza naumati wa wakazi mji wa Korogwe katika viwanja vya Chuo cha Ualimu Korogwe jana.